Monday, December 11, 2017

FANYA MAAMUZI SAHIHI - MR. EMMANUEL WAMBURA

Tunamshukuru Mungu Jumapili hii tumekuwa na ibada ya baraka sana, Mungu alimtumia Mtumishi wake Mr, Emmanuel Wambura, katika kutukumbusha Somo la Kufanya maamuzi sahihi.

 (Pichani ni Mr. Emmanuel Wambura akihubiri)

Mr. Wambura, akiwa na Mtafsiri wake Mchungaji Michael Malabeja, aliwakumbusha washirika, kuwa katika kila jambo wanalolifanya lazima kuna maamuzi mawili yapo mbele yanatakiwa kuchaguliwa, either, maamuzi mazuri, au maamuzi mabaya.

(Pichani ni Mr. Emmanuel Wambura na Mchungaji Michael Malabeja wakihubiri)

Mhubiri alitumia maandiko kutoka kitabu cha Mwanzo 4:1-7 katika kufikisha ujumbe aliotumiwa na Mungu

Mwanzo 4:1-7
 1 Adamu akamjua Hawa mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Kaini, akasema, Nimepata mtoto mwanamume kwa Bwana.
 2 Akaongeza akamzaa ndugu yake, Habili. Habili alikuwa mchunga kondoo, na Kaini alikuwa mkulima ardhi.
 3 Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa Bwana.
 4 Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. Bwana akamtakabali Habili na sadaka yake;
 5 bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana.
 6 Bwana akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?
 7 Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.

 (Pichani, ni washirika wakisikiliza neno la Mungu)


Mchungaji kiongozi, wa kanisa la Msewe Christian Revival Centre, mchungaji Godwin Mujaki alihitimisha kwa kumshukuru Mr. Emmanuel Wambura kwa kuitikia wito wa kufikisha ujumbe Mungu aliokusudia na kusisitiza washirika wautendee kazi ujumbe huo.

(Pichani ni Mchungaji Godwin Mujaki akimshukuru Mr. Emmanuel Wambura.)

Mchungaji Godwin Mujaki, aliwaombea watu wenye matatizo mbali mbali waliohitaji mkono wa Mungu kuingilia kati katika maisha yao.

(Washirika wakifanyiwa maombi)

HAKIKA TULIBARIKIWA SANA KATIKA IBADA HII. KARIBU SANA MSEWE CHRISTIAN REVIVAL CENTRE, KWA MCHUNGAJI GODWIN NA SCOLLA MUJAKI.

KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA NAMBA  :   0752 636641






No comments:

Post a Comment