Saturday, December 16, 2017

MKESHA WA VIPAJI - JIGUNDUE KIPAJI CHAKO

Tunamshukuru Mungu, tumekuwa na mkesha mkubwa, uliowakutanisha wanavyuo wote waliopo Dar Es Salaam kwa pamoja katika tukio kubwa la Kugundua vipaji walivyonavyo.

(Pichani ni wanafunzi wa vyuo mbali mbali Dar Es Salaam, wakimsifu Mungu)

Pia, katika tukio hili la usiku wa kujigundua,  (Talent ovenight Exhibition,), tulikuwa na somo zuri kutoka kwa mchungaji Michael marabeja, 

Pichani ni mchungaji Michael Malabeja Akihubiri

Mchungaji Michael alihubiri somo lililobeba kichwa cha "Vitu ambavyo vinaweza kuchangia usifikie kiwango ambacho Mungu amekuwekea ndani yako".

aliorodhesha baadhi ya vitu hivyo kama

1. Ukosefu wa Utii kwa kitu Mungu alichoweka ndani yako.
2. Hofu ya kushindwa kufanikiwa
3. Kukata tamaa (Kila kitu kizuri kinahitaji uvumilivu)

(Wanafunzi wa vyuo wakimsikiliz mchungaji Michael akiwa anahubiri)

4. Mtazamo"Hakuna mtu anaweza akakuhukumu katika jambo zaidi ya wewe mwenyewe na neno la Mungu"
5. Mtazamo cha hasi (Kuhairisha mambo unayotaka kuyafanya kutokana na mtazamo hasi)
6. Kushindwa mara kwa mara
7. Mtazamo(Mrejesho) wa watu wengine juu ya maisha yako.
8. Kupoteza Muelekeo wa jambo ulilokusudia kulifanya
(1kor 6:12)
9. Kuridhika na mafanikio madogo madogo
(uwezo ni wewe ulivyotakiwa kuwa, ila bado haujafikia ulivyotakiwa kuwa)
10.Kuwa katika mazingira yasiyofaa
11. Kujilinganisha na watu wengine
12. Dhambi

Mchungaji Michael Malabeja, akiwaombea wanafunzi walioamua kuokoka


Katika mkesha huu, kulikuwa na waimbaji mbali mbali waliojumuika pamoja nasi katika usiku wa kujigundua.

 Mwimbaji Bale John akimtukuza Mungu katika mkesha wa kujigundua

 Mwimbaji Sarah Ndosi akimtukuza Mungu katika mkesha wa kujigundua
   


No comments:

Post a Comment