Sunday, January 28, 2018
Tuesday, January 16, 2018
Sunday, January 14, 2018
USILIE MWANGALIE YESU - MCHUNGAJI DAVID MWAKAJINGA
Leo tumekuwa na ibada ya kipekee, ni baada ya kutembelewa na ugeni mkubwa kutoka kanisa la TAG Buguruni.
(Pichani ni Mchungaji David Mwakajinga akihubiri)
Watu wengi walibarikiwa kwa somo zuri la USILIE MWANGALIE YESU.
(Pichani ni Mchungaji David Mwakajinga akiwaombea waumini)
(Pichani ni Mchungaji Godwin Mujaki akiwaombea washirika)
Kwaya ya Eden B kutoka TAG BUGURUNI IKIHUDUMU
Washirikika wakisikiliza neno la Mungu
Timu ya kusifu na kuabudu ya walawi ikihudumu
Washirikika wakisikiliza neno la Mungu
Timu ya kusifu na kuabudu ya walawi ikihudumu
Mchungaji David Mwakajinga na mke wake, pamoja na Mchungaji Godwin Mujaki wakimtukuza Mungu kwa pamoja
Watumishi wa Mungu wakitoa pepa
Baadhi ya watu waliokoka katika ibada ya leo
Saturday, December 16, 2017
MKESHA WA VIPAJI - JIGUNDUE KIPAJI CHAKO
Tunamshukuru Mungu, tumekuwa na mkesha mkubwa, uliowakutanisha wanavyuo wote waliopo Dar Es Salaam kwa pamoja katika tukio kubwa la Kugundua vipaji walivyonavyo.
1. Ukosefu wa Utii kwa kitu Mungu alichoweka ndani yako.
2. Hofu ya kushindwa kufanikiwa
3. Kukata tamaa (Kila kitu kizuri kinahitaji uvumilivu)
4. Mtazamo"Hakuna mtu anaweza akakuhukumu katika jambo zaidi ya wewe mwenyewe na neno la Mungu"
5. Mtazamo cha hasi (Kuhairisha mambo unayotaka kuyafanya kutokana na mtazamo hasi)
6. Kushindwa mara kwa mara
7. Mtazamo(Mrejesho) wa watu wengine juu ya maisha yako.
8. Kupoteza Muelekeo wa jambo ulilokusudia kulifanya
(1kor 6:12)
9. Kuridhika na mafanikio madogo madogo
(uwezo ni wewe ulivyotakiwa kuwa, ila bado haujafikia ulivyotakiwa kuwa)
10.Kuwa katika mazingira yasiyofaa
11. Kujilinganisha na watu wengine
12. Dhambi
(Pichani ni wanafunzi wa vyuo mbali mbali Dar Es Salaam, wakimsifu Mungu)
Pia, katika tukio hili la usiku wa kujigundua, (Talent ovenight Exhibition,), tulikuwa na somo zuri kutoka kwa mchungaji Michael marabeja,
Pichani ni mchungaji Michael Malabeja Akihubiri
Mchungaji Michael alihubiri somo lililobeba kichwa cha "Vitu ambavyo vinaweza kuchangia usifikie kiwango ambacho Mungu amekuwekea ndani yako".
aliorodhesha baadhi ya vitu hivyo kama
2. Hofu ya kushindwa kufanikiwa
3. Kukata tamaa (Kila kitu kizuri kinahitaji uvumilivu)
(Wanafunzi wa vyuo wakimsikiliz mchungaji Michael akiwa anahubiri)
5. Mtazamo cha hasi (Kuhairisha mambo unayotaka kuyafanya kutokana na mtazamo hasi)
6. Kushindwa mara kwa mara
7. Mtazamo(Mrejesho) wa watu wengine juu ya maisha yako.
8. Kupoteza Muelekeo wa jambo ulilokusudia kulifanya
(1kor 6:12)
9. Kuridhika na mafanikio madogo madogo
(uwezo ni wewe ulivyotakiwa kuwa, ila bado haujafikia ulivyotakiwa kuwa)
10.Kuwa katika mazingira yasiyofaa
11. Kujilinganisha na watu wengine
12. Dhambi
Mchungaji Michael Malabeja, akiwaombea wanafunzi walioamua kuokoka
Katika mkesha huu, kulikuwa na waimbaji mbali mbali waliojumuika pamoja nasi katika usiku wa kujigundua.
Mwimbaji Bale John akimtukuza Mungu katika mkesha wa kujigundua
Mwimbaji Sarah Ndosi akimtukuza Mungu katika mkesha wa kujigundua
Monday, December 11, 2017
FANYA MAAMUZI SAHIHI - MR. EMMANUEL WAMBURA
Tunamshukuru Mungu Jumapili hii tumekuwa na ibada ya baraka sana, Mungu alimtumia Mtumishi wake Mr, Emmanuel Wambura, katika kutukumbusha Somo la Kufanya maamuzi sahihi.
(Pichani ni Mr. Emmanuel Wambura akihubiri)
Mr. Wambura, akiwa na Mtafsiri wake Mchungaji Michael Malabeja, aliwakumbusha washirika, kuwa katika kila jambo wanalolifanya lazima kuna maamuzi mawili yapo mbele yanatakiwa kuchaguliwa, either, maamuzi mazuri, au maamuzi mabaya.
Mhubiri alitumia maandiko kutoka kitabu cha Mwanzo 4:1-7 katika kufikisha ujumbe aliotumiwa na Mungu
Mwanzo 4:1-7
1 Adamu akamjua Hawa mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Kaini, akasema, Nimepata mtoto mwanamume kwa Bwana.
2 Akaongeza akamzaa ndugu yake, Habili. Habili alikuwa mchunga kondoo, na Kaini alikuwa mkulima ardhi.
3 Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa Bwana.
4 Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. Bwana akamtakabali Habili na sadaka yake;
5 bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana.
6 Bwana akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?
7 Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.
(Pichani, ni washirika wakisikiliza neno la Mungu)
Mchungaji kiongozi, wa kanisa la Msewe Christian Revival Centre, mchungaji Godwin Mujaki alihitimisha kwa kumshukuru Mr. Emmanuel Wambura kwa kuitikia wito wa kufikisha ujumbe Mungu aliokusudia na kusisitiza washirika wautendee kazi ujumbe huo.
(Pichani ni Mchungaji Godwin Mujaki akimshukuru Mr. Emmanuel Wambura.)
Mchungaji Godwin Mujaki, aliwaombea watu wenye matatizo mbali mbali waliohitaji mkono wa Mungu kuingilia kati katika maisha yao.
(Washirika wakifanyiwa maombi)
HAKIKA TULIBARIKIWA SANA KATIKA IBADA HII. KARIBU SANA MSEWE CHRISTIAN REVIVAL CENTRE, KWA MCHUNGAJI GODWIN NA SCOLLA MUJAKI.
KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA NAMBA : 0752 636641
Sunday, November 26, 2017
ELEWA NGUVU YA TABIA, NA UKUZE TABIA NJEMA - MCH:GODWIN MUJAKI
Siku ya leo ilikuwa ya baraka sana, baada ya Mungu kumtumia mchungaji kiongozi wa kanisa la Msewe Christian Revival Centre , Mchungaji Godwin Mujaki katika kufundisha Somo zuri la Tabia.
(Pichani ni Mchungaji Godwin Mujaki akihubiri.)
Katika mafundisho yake, alitolea mifano mbali mbali ya tabia za baadhi ya watu kwenye biblia, ikiwemo tabia ya Yesu, ambapo alisema kuwa Yesu alikuwa (Mtu wa ibada (Luka 4:16) pamoja na (Mtu wa maombi (Yohana 18:1-2).
(Pichani ni washirika wakisikiriza neno la Mungu)
VITU VYA KUFAHAMU KUHUSU TABIA
1.Tabia yaweza kuwa mbaya au nzuri na pia tabia inaweza ikawa ya kiroho au ya asili.
2. Ni kitendo kinachorudiwa kwa urahisi pasipo kufikilia au kupanga kukifanya
3. Tabia mbaya huongoza katika kushindwa,uwe unajua au haujui
4. Tabia nzuri huongoza kwenye kushinda ikiwa muhusika anajua au hajui
5. Tabia nzuri ni ngumu kuitengeneza, ilanirahisi kukaa nazo
6. Tabia mbaya ni rahisi kuzitengeneza ila ni ngumu kukaa nazo
7. Unapokuwa na tabia njema, ni lazima uwe mlinzi wa tabia hiyo.
1 Wakorintho 15:33
Pichani ni Mchungaji Godwin Mujaki (kushoto) pamoja na mtafsiri wake, Mchungaji Denis Bashurura.
VITU VYA KUZINGATIA
1.Upo hivyo kama ulivyo kutokana na Tabia
2.Tabia nikitu unafanya bila kukusudia na bila kujua
3. Tabia hutokea kwa mtu, kwa kupanga, kwa kupania na kwakujizoesha kufanya jambo hilo hilo bila kukatishwa na mtu
4.Daniel alikuwa na tabia ya kuomba sirini (Daniel 6:10)
5. Imani iliyojengwa juu ya tabia, ni imani isiyoshindwa.
HAKIKA TULIBARIKIWA SANA. KARIBU SANA MSEWE CHRISTIAN REVIVAL CENTRE.
Mawasiliano : +255 752 636 641
WOTE MNAKARIBISHWA.
Subscribe to:
Posts (Atom)