Monday, May 11, 2015

TAMASHA LA KUSIFU NA KUABUDU

TUNAMSHUKURU MUNGU TULIKUWA NA TAMASHA LA KUSIFU NA KUABUDU SIKU YA JUMAPILI. TAMASHA HILI  LILIANDALIWA NA KIKUNDI CHA "THE POWERFUL PRAISE", WATU WENGI WALIJUMUIKA PAMOJA NASI KATIKA SIFA NA KUABUDU, HAKIKA MUNGU ALIONEKANA.

Yohana 4:23Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.












GET READY

WE THANKS GOD FOR THIS WONDERFUL DAY , TODAY WAS CMF(MEN'S) DAY NATIONAL WIDE IN ALL TANZANIA ASSEMBLIES OF GOD CHURCHES.
HERE AT MCRC WE HAD A GREAT SERVICE WHICH WAS HELD BY A MAN OF GOD MR. MWANZALIMA. THE TITLE OF THE MESSAGE WAS Get ready.


WE AS CHRISTIANS WHO ARE WAITING FOR JESUS TO ARRIVE, WE MUST BE READY SO AS WHEN HE COMES HE FIND US WE ARE READY TO GO WITH HIM.

 
SOME THINGS TO CONSIDER

1.There must be a power that will enable you to wait for the Lord
2.The salvation is free, but the life of salvation requires to give your time to Christ
3. In order to get ready , carry your oil(Holy Spirit) MATTHEW 25:1-13
4. Dont ask for simple things, ask for the power to confront hard things









THE POWER OF THE PROMISE

WE THANKS GOD FOR THIS WONDERFUL DAY GOD HAS GRANTED US TO SEE, TODAY WE HAD A GREAT SERVICES WHICH WAS MINISTERED BY PASTOR GODWIN MUJAKI AT MCRC. HE TAUGH ABOUT 



THE POWER OF THE PROMISE

1.Promises in the history
Exodus 34:22
2.God implanted the church for the harvest of the world

GOD PROMISES AS THE PROMISE OF THE HOLY SPIRIT THAT HE WILL COME TO US AFTER JESUS IS GONE, THIS WAS THE PROMISE WHICH JESUS WENT BACK TO HEAVEN , AND THE FOLLOWING ARE THE RESULTS OF BEING FILLED WITH THE HOLY SPIRIT


The results of being filled with the holy spirit

1. A person is impower to testisfy the good news of jesus

2. The gifts of the profets start

3. The falling of the holy spirit 

4. Holyness obdience and rigousness is born

5. The level of revelence to God is born6. The level of diversion to God is born

7. The deciples where speaking in toungue








Sunday, May 10, 2015

UMUHIMU WA UBATIZO WA ROHO MTAKATIFU

Tunamshukuru Mungu tulikuwa na ibada ya baraka sana iliongozwa na mtumishi wa Mungu mama mchungaji Scolla Mujaki. alihubiri ujumbe mzuri sana juu ya 


SABABU TANO ZA KUAMINI KUWA UBATIZO WA ROHO MTAKATIFU NI MUHIMU KWA KANISA LA SASA.Sababu hizo ni kama ifuatavyo

1.Ulikuwa ni ujumbe wa kwanza kwa Mtume Paulo kwa wale wanafunzi kumi na mbili kwa Effeso
MATENDO YA MITUME 19:1-7

2.Ulikuwa ni ujumbe wa mwisho wa Yesu katika kanisa
MATENDO YA MITUME 1:8

3.Hata Maria mama yake Yesu alihitaji nguvu za Roho Mtakatifu
MATENDO YA MITUME 1:13-14

4.Ndio ilikuwa ahadi pekee katika biblia inayopewa umuhimu
MATENDO YA MITUME1:4

5.Yesu mwenyewe aliamua kufanya huduma kwa nguvu na upako katika roho mtakatifu
Luka 3:21





Thursday, May 7, 2015

ROHO MTAKATIFU

Tunamshukuru Mungu kwa siku ya leo , tumekuwa na ibada njema sana iliyo ongozwa na mtumishi wa Mungu MCHUNGAJI ERASTO KIHONGO. Alifundisha juu ya Roho MtakatifuAndiko kuu lilikuwa Matendo 1:8

MAMBO MATATU YA KUJIFUNZA KWENYE MATENDO 1:8

1.Ahadi za nguvu zinazotokana na Roho Mtakatifu

2. Makusudi ya nguvu za Roho Mtakatifu kuwa shahidi

3. Muongozo baada ya kupokea Roho na kuwa shahidi unaelekea wapi

SIFA ZA ROHO MTAKATIFU

1. Yeye ni wa milele Waebrania 9:14

2. Uungu wa kila mahali  Zaburi 139:1-10

3. Anazosifa za kuwa na nguvu zote Luka 1:35

4. Anajua yote 1 kor 2:10-11 

5. Utendaji wake pamoja na Mungu Mwanzo 1:2 Ayubu 33:4

6. Anazaa upyaYohana 3:5-8

7. Anacheo sawa na Baba na Mwana1 kor 12:4-6

    Wakorinto 13:14Mathayo 28:9 Ufunuo 1:4







UJAZO WA ROHO MTAKATIFU

Tunamshukuru Mungu Jumapili hii Mungu ameonekana kwa namna ya tofauti sana, Mchungaji Eliya lugwami alihubiri juu ya Roho Mtakatifu.Moja ya kitu alicho sema ni "Wajibu wa mkristo baada ya kumpokea Yesu kristo,ni kupokea Roho wa Mungu"  hii ni kweli maana kama ilivyoandikwa katika kitabu cha " Matendo ya mitume 1: 8 Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi." 

Roho Mtakatifu anakazi nyingi kwa mtu aliyeokoka, kama,
1. kututia nguvu/ kutuwezesha
2. Kutuongoza
3. Kutuchukua na kututia kwenye kweli yote
4. Kutukumbusha
5.Kutuombea
6. Kutuwezesha kujua tuliyo kirimiwa
7. Kutupasha habari ya mambo yajayo
pia unaweza ukapitia haya maandiko kwa uwelewa zaidi










Saturday, April 4, 2015

ROHO MTAKATIFU

Tunamshukuru Mungu Leo tumekuwa na ibada ya baraka sana iliongozwa na mtumishi wa Mungu mama mchungaji Scolla Mujaki. WAtu wengi waliokoka na kufunguliwa, wengi walijaa Roho Mtakatifu.
Kichwa cha ujumbe kilikuwa ni "ROHO MTAKATIFU".
KWA NINI TUJAZWE NA ROHO MTAKATIFU?
1.Tunajazwa na Roho Mtakatifu ili tuweze kuishi maisha kama aliyoishi Yesu
2. Ili tuweze kuishi maisha safi na Matakatifu
3. Mungu anataka tuwe na upendo
Bila Roho Mtakatifu atutaweza kutimiza mapenzi ya Mungu.










KUTENGENEZA TABIA NJEMA

Tunamshukuru Mungu Jumapili ya leo tumekuwa na ibada njema sana iliyoendeshwa na mtumishi wa Mungu Andrea Benedictor. Mungu alimtumia kwa namna ya kipekee. Ujumbe aliofundhisha Jumapili ya leo ni "KUTENGENEZA TABIA NJEMA"
Maana ya tabia
 Mazoea(kufanya jambo mara kwa mara na baadaye inakuwa sehemu ya maisha)inakuwa ngumu kuacha.
Mwenendo-staili ya maisha,
Desturi –tabia ya kurithi katika jamii ya mahali fulani.Mfano. Wachaga wana tabia ya kupenda fedha,Wahaya wanapenda kusoma
Wanasaikolojia
Tabia ni matendo,mienendo au hulka zinazoweza kuonekana wazi,kupimwa na hata kuchunguzika kwa misingi ya kisayansi(tafiti) na kawaida.
Ingawa misingi ya tabia zote ni mawazo,imani,fikra na mitazamo isiyoonekana LAKINI Matokeo yake ni kuonekana kwa vitendo.
Hivyo mawazo ya aina fulani uendelea kwenye ufahamu wa mtu na matokeo yake ni  vitendo.1Kor.15:33 “Msidanganyike,mazungumzo mabaya,huharibu tabia njema)
Ki-Biblia
Tabia mbaya inaitwa Mambo ya mwilini,tabia ya asili,ya dunia,kibinadamu,kishetani,mataifa.
Yakobo 3:15
(Hekima hiyo siyo ile ishukayo kutoka juu, bali ni ya dunia, ya tabia ya kibinadamu, na Shetani.)Tabia nzuri inaitwa Tabia ya Rohoni,Ki-ungu.Mara nyingi huioni kwako bali watu wengine ndio wanaiona.
I.TABIA MBAYA HUZAA MATATIZO MENGI
 1. Jamii inakutenga,inakukimbia
2. Kukosa fursa(Kazi,kuinuliwa-promotion,kufukuzwa kazi,kukosa tenda)
3.Kuzuia maendelea-Kwenye nafasi fulani,Mkuu wa Idara fulani(“achana idara”)
4.Kuwa kwazo-Kila siku unakuwa unakwaza watu,ni wewe tu unayesababisha
Matatizo.Watu wanaanza kufunga na kuomba kwa ajili ya makwazo yako
5.Unajizuilia Baraka za Mungu.Mungu akikuangalia akubariki kwa Baraka zake,
ili ufanyike jibu kwa watu,anaona tabia ya ubinafsi,uchoyo,Anaona madhara
hasi Badala ya watu kubarikiwa anaona wananyanyasika
6. Dharau na fedheha.Ukiwa na tabia mbaya utadharaulika na jamii inayokuzunguka
III:ACHA TABIA MBAYA
A.Omba Mungu akufunulie tabia zako mbaya.Uliza mtu wako wa karibu akueleze.
B: Zichukie tabia mbaya ulizo nazo
C: Kubali Ushauri
B.Amua kuanza kuishi maisha ya kupendeza.
Wafilipi.4:8
Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.
C:Omba uwezesho wa Roho Mtakatifu.
Warumi 12:1-2
1 Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.
 2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.






KUBADILISHWA NA DHIKI

Tunamshukuru Mungu Jumapili ya leo tumekuwa na ibada ya kipekee iliongozwa na mchungaji wa kimataifa Yohan Suleiman. Alihubiri ujumbe unaoitwa "kubadilishwa na dhiki". Watu wengi wamekuwa wakipitia dhiki mbali mbali maishani mwao, wanasahau kuwa Mungu yupo anaeweza kubadilisha dhiki wanazopitia kuwa furaha. Tumtumaini Mungu katika maisha yetu naye atatubadilisha katika dhiki zetu. Jumapili hii watu wengi walibalikiwa na ujumbe huu, wengi waliokoka na wagonjwa waliponywa.





Thursday, April 2, 2015

MAOMBI YA VIKUNDI

Tunamshukuru Mungu kwa Jumapili ya leo, ameweza kuonekana kwa namna ya ajabu sana, pia Mungu ametuwezesha kufanikisha zoezi la kupanga vikundi vya maombi. Ili mambo yatendeke tunahitaji kuomba kwa bidii sana
1 Wafalme 18:24 Nanyi ombeni kwa jina la Mungu wenu, nami nitaomba kwa jina la Bwana; na Mungu yule ajibuye kwa moto, na awe ndiye Mungu. Watu wote wakajibu wakasema, Maneno haya ni mazuri.